-
90
pages
-
Swahili (generic)
-
Ebooks
-
2022
Description
Mstahamilivu hula mbivu, mtaka cha uvunguni sharti ainame, na mchumia juani hulia kivulini. Ni machache ya maadili yamuongozayo binti Malaika katika safari yake ya kutimiza ndoto zake. Kujiendeleza kielimu ndiyo ndoto yake kuu. Kwa vile Mungu hamtupi mja wake, anabahatika kwenda ughaibuni kitaaluma. Ni safari inayomtenganisha na mpenzi wake, Ben. Lakini Ben anaahidi kumsubiri hadi afuzu masomo yake. Katika kipindi hiki cha utengano, dunia inawapangia mambo mengine kabisa, ni utengano unaotishia kulisumu penzi lao. Majaribu hayeshi, vishawishi ni vingi. Penzi lao linayumba, linatishia kudumbukia kwenye dimbwi la damu. Lakini Malaika haliachii penzi lake kwa Ben, analipigania kishujaa. Ben pia anaingia vitani kulipigania penzi la Malaika. Je, watashinda vita hivi vya kimapenzi?
-
Publié par
-
Date de parution
22 septembre 2022
-
EAN13
9789987080182
-
Langue
Swahili (generic)
-
Poids de l'ouvrage
1 Mo